Jumamosi, 27 Julai 2013

NILIJUA TU KWAMBA WANAFIKI WATAFURAHIA MATESO YANGU" ....AGNESS MASONGANGE


VIDEO Queen ambaye hivi karibuni alidaiwa kukamatwa na madawa yanayosadikiwa ni ya kulevya ‘unga’ nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’, Agness Gerald ‘Masogange’ amefunguka kuwa alijua watu wengi watafurahia kilichompata kwa kumuongelea kila wakati.
Akizungumza na mwanahabari wetu kwa njia ya simu akiwa Sauzi, Masongange ‘alishauti’ kuwa watu wengi wanamuongelea vibaya bila kujua nini kilichompata  hivyo anaamini hata marafiki zake wa karibu wamefurahia tatizo alilopata.

“Najua kabisa kuna watu wengi wamefurahia tatizo nililopata lakini watambue kuwa kila mtu anaweza kupata tatizo hivyo wapunguze kuongea sana bila kujua ni kitu gani kilichotokea juu yangu,” alisema Masogange ambaye atapanda kizimbani kwa mara ya pili mwezi ujao

UPDATE: Baada ya tuhuma, hatimaye Jennifer Kyaka (Odama) atoa ushahidi wa kwenda nje.

UPDATE: Baada ya tuhuma, hatimaye Jennifer Kyaka (Odama) atoa ushahidi wa kwenda nje.
  • UPDATE: Baada ya tuhuma, hatimaye Jennifer Kyaka (Odama) atoa ushahidi wa kwenda nje. 1
  • UPDATE: Baada ya tuhuma, hatimaye Jennifer Kyaka (Odama) atoa ushahidi wa kwenda nje. 2
  • UPDATE: Baada ya tuhuma, hatimaye Jennifer Kyaka (Odama) atoa ushahidi wa kwenda nje. 3
Baada ya wadau mbalimbali kuanza kuhoji kuhusu uhalisia wa safari za mwigizaji Jennifer Kyaka (Odama) kwenda ulaya ambaye picha zake kadhaa zilizotolewa mtandaoni wiki chache zilizopita zikimtuhumu kuwa huwa haendi nje ya nchi bali anakuwepo nchini kwa lengo la kutafuta “kiki” na kutengezeza picha hizo kwa program maalumu ya kompyuta, hatimaye jana kupitia mtandao mmoja wa kijamii aliweka picha zake mpya zinazomuonesha nchini Qatar katika maduka mbalimbali na kwenye uwanja wa ndege wa nchi hiyo.
 Picha hizi zimekuja kama ushahidi na majibu ya mwaswali yaliyokuwa yakiulizwa na wadau wengi kuhusu mwanadada huyu. Tazama picha hizi hapo

PICHA: Kajala masanja akiwa afrika ya kusini, atembelea shule ya uigizaji

PICHA: Kajala masanja akiwa afrika ya kusini, atembelea shule ya uigizaji
  • PICHA: Kajala masanja akiwa afrika ya kusini, atembelea shule ya uigizaji 1
  • PICHA: Kajala masanja akiwa afrika ya kusini, atembelea shule ya uigizaji 2
  • PICHA: Kajala masanja akiwa afrika ya kusini, atembelea shule ya uigizaji 3
  • PICHA: Kajala masanja akiwa afrika ya kusini, atembelea shule ya uigizaji 4
Juzi mwigizaji wa bongo movies  Kajala aliondokoka nchini kuelekea Afrika ya kusini kwa ajili ya safari binasfi ambayo pamoja na mambo mengine alitembelea  shue ya uigizaji ya AFDA (AFDA the South African School of Motion Picture Medium and Live Performance)  iliyopo nchini humo.
Tazama hapo picha kadhaa za msanii huyo nchini humo

Wakazi ajibu “diss” ya TID

wakazi
Baada ya TID kuandika:
Wakazi ataimba wimbo gani, anaenda kuonyesha kofia zake za marekani#mzee kasema#radarworththisshit#watuwabaya#msiwemaf**a.”
katika mtandao wa Twitter kufuatia Wakazi kualikwa kuperform katika eviction show ya Big Brother Africa, Wakazi amemjibu kwa kusema:
“Sasa ntamjibu nini, anaongea vitu asivyovifahamu, yeye hapo akimuona Wakazi anaona kofia za Marekani sasa mtu kama huyo utaongea naye? The greatest ignorance ya mtu ni pale anapoamua kudiss kitu ambacho hakijui au hajakifahamu bado vizuri , mtu kama huyo huwezi kuanza kubishana naye, na yeye ananiona mimi Mmarekani, wakati mimi ni Mtanzania, angekaa miaka mitatu Ulaya au Marekani angejiona na yeye ni mtu wa huko kwa jinsi upeo wake ulivyo.”

Majina ya askari saba wa Tanzania waliokufa kwenye shambulio la ghafla mjini Darfur

jem-force
Majina ya askari saba wa Tanzania waliokufa kwenye shambulio la ghafla mjini Darfur yamepatikana.
Askari hao waliokufa ambao walikuwa kwenye vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa huko nchini Sudan ni Sajenti Shaibu Othuman, Koplo Oswald Chaula, Koplo Mohamed Juma, Koplo Mohamed Chikilizo, Pte. Rodney Ndunguru, Pte. Peter Werema na Pte. Fortunatus Msofe.
Taarifa zilizopatikana kwenye mtandao ni kwamba askari hao walikwenda kujaribu kumwokoa mwenzao (ambaye hakutajwa) ambaye alisemekana kutekwa na vikosi vya waasi nchini humo.Wakati wakijiandaa, ghafla walizingirwa na askari hao waasi na kisha kushambuliwa kwa risasi hadi kufa.
Haikufahamika hali ya askari huyo ambaye alidaiwa kutekwa kama bado yu hai ama ni miongoni mwa waliokufa.
Mungu azilaze roho za askari wetu mahali pema peponi, Amina.

Hot: Waraka wa Kala Jeremiah kuhusu Mh. Edward Lowassa

Kala-Jeremiah
TANGAZO KWA UMMA
MIMI KALA JEREMIAH NILIKUWA MSANII WA KWANZA TANZANIA KUMSEMA MHESHIMIWA EDWARD LOWASA KUPITIA WIMBO WANGU UITWAO WIMBO WA TAIFA BAADA YA MHESHIMIWA KUKUMBWA NA KASHFA YA UFISADI WA RICHMOND.KWA KIPINDI KILE KILA MMOJA WETU ALIHAMAKI SANA NA KUONA KWELI MZEE WA WATU NI FISADI.KWENYE WIMBO HUO KUNA MISTARI NILISEMA. mi siyo mwana siasa sisubiri tume ichunguze nistaafu ka Lowasa.
KWA KUWA MIMI NI MZURI SANA KWENYE KUFANYA UCHUNGUZI BINAFSI NILITUMIA MUDA MWINGI SANA KULICHUNGUZA SWALA HILI LA KASHFA HII NA BAADAE NILIGUNDUA KUWA NI SWALA LA KISIASA.NA YALIKUWA NI MAPITO AMBAYO MWANADAMU YOYOTE HUPEWA MUDA WA KUPITIA MAGUMU ILI KUPIMWA IMANI YAKE KWA MUNGU.
BAADA YA KUGUNDUA HAYO MWAKA JANA NILITENGENEZA WIMBO UNAOITWA AZIMIO LA ARUSHA AMBAO UPO KWENYE ALBUM YANGU YA PASAKA AMBAYO IKO SOKONI TOKEA MWAKA JANA. KATIKA WIMBO HUO WA AZIMIO LA ARUSHA NILIANDIKA MISTARI IFUATAYO. walipiga dili waka msakizia lowasa ili kuficha siri kali.NILIANDIKA MSTARI HUU BAADA YA KUFANYA UCHUNGUZI NA KUJIRIDHISHA KUWA MHESHIMIWA NI KIONGOZI BORA SANA NA HASA KWA UAMUZI WAKE WA KUJIUZULU BILA SHINIKIZO KUBWA NA WAKATI KWA NAFASI ALIYOKUWA NAYO YA UWAZIRI MKUU ALIKUWA NA UWEZO WA KUGOMA KUJIUZULU NA HASA KWA KUWA HAKUWA FISADI KAMA ILIVYOSEMWA.
MWEZI WA TATU MWISHONI MWAKA HUU NILITOA WIMBO UNAOKWENDA KWA JINA LA KARIBU DAR AMBAKO NILISEMA dar es salam ingekuwa nchi Rais angekuwa Lowasa huku watu washashtukia kuna mchezo kwenye siasa HAPA NILIKUWA NAMAANISHA KUWA WATU WENGI WANAOISHI DAR WANAWAHI KUJUA MAMBO YA WANASIASA KWA KUWA WANASIASA WANAISHI HUKU LAKINI PIA WATAFITI WENGI WA MAMBO YA KISIASA WANAISHI HUKU KWA HIYO NI RAHISI ZAIDI KUUJUA UKWELI MAPEMA.
NAAMINI KUONDOKA KWA LOWASA KWENYE UWAZIRI MKUU KUMEZOROTESHA MAENDELEO YA TAIFA KWA KIASI FLANI
NDUGU ZANGU WATANZANIA NI WAZI KUWA LOWASA NI JEMBE TENA JEMBE LA KAZI KUMBUKENI BILA LOWASA KUSINGEKUWA NA SHULE ZA KATA TANZANIA,NA ANGEENDELEA KUWEPO MADARAKANI ALIKUWA NA MPANGO WA KUANZA MCHAKATO WA ZAHANATI ZA KATA.IKUMBUKWE PIA LOWASA NDIYE ALIYESIMAMIA UJENZI WA CHUO CHA UDOM TENA KWA PESA ZA KITANZANIA BILA KUOMBAOMBA VIMIKOPO.
MRADI WA MAJI KUTOKA MWANZA KWENDA SHINYANGA NI KAZI YA LOWASA. ZIPO KAZI NYINGI AMBAZO NIKIZITAJA ZOTE NAWEZA KUJAZA UKURASA.NACHOJARIBU KUSEMA HAPA NI KWA KUWA MIMI NI MSANII NA NI KIOO CHA JAMII NINGEOMBA WEWE MWANAJAMII CHUKUA HATUA YA KUFANYA UCHUNGUZI BINAFSI KUHUSU LOWASA.BILA KUFUATA MKUMBO WA KISIASA NAAMINI UTAKUBALIANA NA MIMI KUWA LOWASA NI JEMBE.
MIMI HUWA NAPENDA KUSOMA VITABU VYA WANAHARAKATI NA KUNA KITABU KIMOJA NILIKIPITIA CHA MWANAHARAKATI KUTOKA ITALY AITWAE NICCOLO MACHIAVELLI AMBAYE ALIZALIWA MWAKA 1469 NA KUFARIKI 1527. KATIKA ENZI ZA UHAI WAKE ALIWAHI KUANDIKA VITABU KADHAA LAKINI KATI YA VITABU HIVYO KITABU KIITWACHO THE PRINCE NDICHO KILIMPA HESHIMA KUBWA SANA KWA KUWA ALIIKOSOA SERIKALI YA KIFALME YA KIPINDI HICHO KITU AMBACHO HAKIKUWA RAHISI KWA MTU KUFANYA HASA IKIKUMBUKWA KUWA ENZI ZA UFALME ZILIKUWA ENZI ZA UBABE. KATIKA MANENO KUTOKA KWENYE KITABU HICHO AMBAYO NINGE PENDA KUKUSHIRIKISHA WEWE NDUGU YANGU MTANZANIA NI MANENO YAFUATAYO MACHIAVELLI ALIANDIKA HIVI. kuna kipindi ambacho mataifa yanapita katika vipindi vigumu. na kwa kipindi hicho kigumu mataifa hayo yatahitaji sana kupata kiongozi mwenye kuweza kuchukua maamuzi magumu,na ambaye hatakuwa chini ya sauti ya mtu mwingine, na ambaye ataweza kuyatekeleza maamuzi magumu kwa haraka hata kama ni kwa kuwaumiza wachache ili wengi wawe huru.atakayekuwa tayari kutekeleza jambo baya ili likapita na kusahaulika na atakayetekeleza mambo mazuri kwa muda mrefu na yakaendlea kukumbukwa.kiongozi huyo atatakiwa kuchagua kuogopwa ama kupendwa lakini ni bora akachagua kuogopwa lakini akitenda haki kwa wananchi husika.HAYO NI BAADHI YA MANENO ALIYOANDIKA MACHIAVELLI KWENYE THE PRINCE KITABU AMBACHO KILIMPELEKEA KUITWA NA MFALME NA KUPEWA NAFASI YA JUU YA UONGOZI KATIKA SERIKALI HIYO YA KIFALME.
KWA MAONI YANGU NADHANI TAIFA LETU LIMEPITIA VIPINDI VIGUMU KADHAA NA KWA MANENO YA BWANA MACHIAVELLI NADHANI KIONGOZI ANAYEFAA AMBAYE ANAWEZA AKACHUKUA MAAMUZI MAGUMU NA AMBAYE HAWEZI KUWA CHINI YA SAUTI YA MTU MWINGINE NI MHESHIMIWA EDWARD NGOYAI LOWASA.

Vilabu vinne vyapigwa marufuku Nigeria

Muke Umeh, mwenyekiti wa kamati andalizi ya shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria NFF
Vilabu vinne ambavyo vilihusika na njama ya kupanga matokeo ya mechi vimepigwa marufuku nchini Nigeria.
Katika mechi moja klabu moja iliilaza nyingine magoli 79-0 na magoli 67-0 katika mechi ya pili.
Jumla ya magoli 146 zilifungwa katika mechi hizo mbili, idadi ambayo inaingia katika vutabu vya kumbukumbu kama mechi iliyokuwa na idadi kubwa zaidi ya magoli duniani.
Klabu ya Plateau United Feeders iliilaza timu ya Akurba ili hali timu ya Polisi ya Machine FC kwa upande wake ikailaza Bubayaro magoli 67-0.
Mwenyekiti wa kamati andalizi ya shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria, Muke Umeh amesema ufisadi na ulaghahi wa kiwango hicho hakiwezi kukubalika katika soka ya sasa.
Umeh ametangaza kuwa baada ya mkutano wa kamati hiyo, ilibainika wazi kuwa vilabu hivyo vina kesi ya kujibu na hivyo vyote vinne vimepigwa marafuku ya kushiriki katika mecho yoyote, hadi uchunguzi utakapokamilika.

Mchezo unaopendwa na wengi

Mechi ya soka katika mtaa mmoja nchini Nigeria
Kabla ya mechi hiyo vilabu vya Plateau United Feeders na Police Machine vilikuwa na alama sawa na vilikuwa vikipania kupandishwa daraja hadi ligi daraja ya pili.
Feeders ilipata magoli 72, katika kipindi cha pili ili hali Machine nao wameripotiwa kufunga magoli 61 katika kipindi cha mechi yao.
Kufuatia matokeo hayo Plateau ilimaliza ya kwanza kwenye msimamo wa ligi na idadi kubwa ya magoli ikifuatwa na timu hiyo ya polisi.
''Tutachunguza sakata hii na kuwachukulia hatua kali wote waliohusika'' Alisema Ummeh.
Mkurugenzi wa michezo na mashindano wa Shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria, Dkt. Mohamed Sanusi, amekariri tangazo lililotolewa na mwenyekiti wa kamati andalizi kuwa waliohusika wataadhibiwa vikali.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na NFF, vilabu vilivyohusika, wachezaji,, maafisa wa kiufundi wa timu na wasimamizi wa mechi hiyo watakaopatikana kuhusika kwa njia moja au nyingine, katika kashfa hiyo ambayo imetajwa kuwa mbaya zaidi katika historia ya soka nchini Nigeria watachukulia hatua kali za kisheria.

Mashirika yahofia hali ya kibinadamu DRC


Mashirika ya misaada yanataka UN kujali hali ya raia wakati mgogoro DRC ukiendelea
Mashirika ya misaada katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo , yameelezea hofu kuhusu operesheni ya kijeshi inayopangwa na Umoja wa Mataifa yakisema kuwa itavuruga zaidi hali ya kibinadamu nchini humo.
Mashirika hayo yanayoshughulikia wakimbizi yanasema kuwa umoja wa mataifa unastahili kutumia mbinu salama zaidi ili kuwaokoa raia kutokana na athari za hatua ya kikosi cha Umoja huo kuingilia kati mzozo unaoendelea.
Umoja huo una zaidi ya wanajeshi elfu tatu.
Tayari wanajeshi wameanza kushika doria
Shirika la misaada la Medecins Sans Frontieres hapo awali lililalamika kuwa kuwepo kwa vikosi vya UN kunaweza kutatiza shughuli za shirika hilo kuwapa msaada waathiriwa wa mgogoro huo kwani huenda wakalengwa kwa mashambulizi na wapiganaji.
Baraza la umoja wa mataifa baadaye leo litajadili hali nchini DRC ambako zaidi ya watu milioni mbili unusu wameachwa bila makaazi kutokana na mzozo huo.

Utulivu wahimizwa nchini Sudan Kusini

Marekani na Umoja wa Ulaya wamewataka viongozi wa Sudan Kusini kuendeleza hali ya utulivu na kuzuia vitendo vya ghasia baada ya Rais Salva Kiir kulivunja baraza la mawaziri akiwemo naibu wake.
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini
Marekani imesema imesikitishwa sana na hali ya kuhatarisha utulivu wa taifa hilo changa duniani.
Bwana Kiir alilivunja baraza la mawaziri siku mbili zilizopita katika kile kinachoonekana kuwa ni kugombea madaraka kati yake na makamu wa rais Riek Machar.
Mabomba ya mafuta Sudan Kusini
Sudan Kusini yenye utajiri mkubwa wa mafuta ilipata uhuru wake kutoka Sudan mwaka 2011 baada ya miaka mingi ya mgogoro kati ya nchi mbili hizo.
Vikundi mbalimbali vyenye silaha vimeendeleza harakati zao nchini humo.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Sudan Kusini Mayek Makol amesema Rais Kiir anafanya mashauriano akipanga kuunda serikali mpya.
Hata hivyo amekataa kusema mashauriano hayo yatachukua muda gani.
"huenda yakachukua siku tatu, nne, au wiki moja", amesema.
Kwa wakati huu wafanyakazi waandamizi wa umma, wanaendesha shughuli za serikali ya nchi hiyo ambayo ni ya mwisho kwa maendeleo duniani.
Katika taarifa yake, wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema:" Ni muhimu kwa Sudan Kusini kubaki na mtazamo wake wa ukweli iliouonyesha wakati wa siku ya uhuru wake miaka miwili iliyopita."
Zaidi ya watu milioni 1.5 waliuawa na wengine zaidi ya milioni nne kukosa mahali pa kuishi wakati wa mgogoro kati ya Sudan Kusini, ambako watu wengi ni Wakristo au kufuata imani za dini za kimila, na waislam wenye kuzungumza Kiarabu , Sudan kaskazini.
Lakini nchi hiyo imepata matatizo sugu ya kiuchumi tangu wakati huo na kuimarika kwa uchumi wake kumecheleweshwa na mvutano juu ya mpaka na mafuta kati yake na majirani zao Sudan Khartoum.

Ijumaa, 26 Julai 2013

MAAJABU YA DUNIA!: ANGALIA WATOTO HAWA WA AJABU WALIOZALIWA!!! CHEKI PICHA HIZI

twin-2


Watoto mapacha wa kiume wamezaliwa huko India wakiwa na vichwa viwili katika mwili mmoja kitu ambacho inasemekana ni nadra sana kutokea.twin-1


Madaktari wamesema wanaamini wanauwezo wa kuokoa maisha ya watoto hao ambao wamezaliwa Jumatano (July 24) huko Jaipur, Rajasthan India.
Kwa mujibu wa taarifa ya Daily Mail, nervous system ya watoto hao imetengana wakati uti wa mgongo umeungana na pia wanashare sehemu ya ubavu.
Dr. S.D. Sharma, wa J.K. Lone Hospital amesema tatizo kama hilo ni nadra sana kutokea hususan kwa watoto wa kiume, na linafahamika kama ‘Dicephalic Parapagus’. Aliongeza kuwa tukio hilo ni la pili kutokea India.
Daktari huyo aliendelea kusema kuwa mara nyingi watoto wenye ‘Dicephalic Parapagus’ huzaliwa wakiwa wamekufa, na mara nyingi hutokea kwa watoto wa kike. Kwa mujibu wa Sharma alisema kuna uwezekano wa kuokoa maisha ya mapacha hao.

twin-3

Tatizo kama hilo lililowahi kutokea kwa mapacha wa kike kutoka Sudan mwaka (2011) ambao waliozaliwa wakiwa wameungana vichwa. Watoto hao Rital na Ritag Gaboura walifanikiwa kutenganishwa salama japo kwa tatizo kama lao uwezekano wa kupona hua ni kwa mmoja kati ya million kumi


 twin-4


Rital na Ritag Gaboura wa Sudan baada ya kutenganishwa
Inasemekana tatizo la mapacha kuzaliwa wameungana hutokea mara moja kati ya watoto 100,000 wanaozaliwa.

TUKIO LILILOJIRI JIJINI DAR: MTU MMOJA AFARIKI DUNIA KWA KUPIGWA RISASI, SOMA HAPA

Wananchi wakibeba mwili wa marehemu baada ya kuuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana.
Mwanaume mmoja ambaye hakujulikana jina lake mara moja, muda mfupi uliopita ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana eneo la Tegeta jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, 
wauaji ni wanaume wawili waliokuwa katika pikipiki maarufu kama 'Bodaboda'. Marehemu alikuwa akishuka katika gari lake aina ya Toyota Mark II yenye namba za usajili T 508 ADY ndipo alipopigwa risasi kadhaa.

Papa apinga madawa ya kulevya

Baba mtakatifu akiwa katika ziara yake nchini Brazil
Kiongozi wa kanisa katoliki, Baba mtakatifu Francis, amekosoa vikali mipango ya kutaka kuhalalisha madawa ya kulevya Amerika ya Kusini.
Aliyasema hayo wakati alipotembelea klikini mpya ya kuwatibu waraibu wa dawa za kulevya mjini Rio de Janeiro.
Vyanzo vya matumizi mabaya ya madawa ya kulevya lazima vitatuliwe, alisema papa katika siku ya tatu ya ziara yake nchini Brazil.
Uruguay inakaribia kuidhinisha uuzaji wa Marijuana au Bhangi huku baadhi ya nchi katika kanda hiyo zikitafakari hatua sawa na hiyo.
Awali Papa Francis mzaliwa wa Argentina alishiriki misa yake ya kwanza katika ziara yake katika kanisa la Our Lady of Aparecida.
Aliwaonya maelfu ya waumini dhidi ya kukumbatia sana pesa, mamlaka na raha za dunia.
Baada ya ziara yake eneo la Aparecida, nchini Brazil Papa alirejea mjini Rio de Janeiro.
Wakati wa ufunguzi wa kliniki ya kutoa matibabu kwa waraibu wa madawa ya kulevya, aliwakumbatia waliokuwa watumizi wa dawa hizo, huku akiwasikiliza wakisimulia yaliyowakumba wakati wa uraibu wao.
"ni muhimu kukabiliana na vyanzo vya matumizi mabaya ya madawa ya kulevya, kuhakikisha haki na kuwafunza vijana kuhusu umuhimu maadili mazuri katika jamii, kuwasaidia wanaokabiliwa na matatizo na kuwapa matumaini,'' alisema Papa.
Papa Francis pia alionya dhidi ya mipango ya kuhalalisha madawa ya kulevya katika kanda ya Amerika ya Kusini huku akiwalaani walanguzi wa madawa hayo.

Fabregas asema hataki kurejea England

Mcheza kiungo wa Barcelona Cesc Fabregas amesema hana nia yoyote ya kuihama klabu hiyo na kurejea tena nchini England.
Hayo ni kwa mujibu wa kocha wake Tito Vilanova.
Klabu ya Manchester United siku ya Jumatatu iliwasilisha ombi la kutaka kumasajili nahodha huyo wa zamani wa Arsenal, kwa kitita cha pauni milioni ishirini na tano, lakini Vilanova amesema mchezaji huyo anataka kusalia nchini Uhispania kwa sasa.
''Ni ishara nzuri kwa klabu yoyote kupata maombi kutoka kwa vilabu vingine, vinavyotaka kuwasajili wachezaji wake, lakini Fabregas amesema anataka kusalia'' Alisema kocha huyo.
Vilanova ameongeza kusema kuwa'' Fabregas hataki kujiunga na timu zingine kwa sababu ya pesa au kutokana na muda wake wa kucheza uliosalia. Anafahamu huku kuna ushindani mkali, lakini ni uamuzi wake kusalia na Barcelona. Kwa sasa nimetulia''.
Kufikia sasa Barcelona halijasema lolote rasmi kuhusiana na ombi hilo la Manchester United, ambalo linaaminika kuwa chini ya dhamana kamili ya mchezaji huyo.
Fabregas alikuwa mchezaji mchanga zaidi wa Arsenal wakakti aliocheza dhidi ya Rotherham United wakati wa mechi ya kombe la ligi mwaka wa 2003 akiwa na miaka kumi na saba na siku mia moja na sabini na saba.
Alikuwa miongoni mwa wachezaji wa Arsenal walioishinda timu ya Manchester United kupitia mikwaju ya penalti kwa fainali ya kombe la FA mwaka wa 2005.
Vile vile Fabregas, anaichezea timu ya taifa ya Uhispania na aliisaidia kunyakua kombe la dunia na pia kuwa mabingwa wa bara Ulaya mara mbili.
Alijiunga na Arsenal mwaka wa 2003 akiwa na umri wa miaka kumi na sita.
Fabregas aliichezea Arsenal mechi 303 na kufunga magoli 57, kabla ya kusajiliwa na Barcelona kwa kitita cha pauni milioni 25.4 kwa mkataba wa miaka mitano kwa wa 2011

Kiamsha kinywa ni muhimu kwa moyo wako!

 

Watu wanapaswa kula kiamsha kinywa ili kuweka mioyo yao katika hali nzuri , kulingana na utafiti uliofanywa nchini Marekani.
Utafiti wao uliowahusisha wanaume 27,000 ulionyesha kuwa wale wasiokula kiamsha kinywa wako katika hatari ya kupata matatizo ya moyo.
Kikundi hicho cha wataalamu katika chuo kikuu cha Havard kitivo cha afya ya umma,kilisema kuwa kukosa kiamsha kinywa kunasababisha mwili kutumia nguvu nyingi zaidi kuliko kawaida.
Taasisi ya matibabu ya moyo Uingereza inasema kuwa kiamsha kinywa huwazuia watu kula vitu vyenye sukari kabla ya chakula cha mchana.
Wanaume waliofanyiwa utafiti wako kati ya umri wa miaka 45-82, na walichunguzwa kwa miaka 16. Wakati wa utafiti huo, zaidi ya watu 1,500 waliathirika kutokana na mshtuko wa moyo.
Hata hivyo, watu waliokosa kiamsha kinywa wako katika hatari kubwa ya kupata matatizo ya moyo kwa asilimia 27 kuliko wale wanaokula asubuhi.
Hata hivyo watafiti walizingatia mambo kama uvutaji sigara na kufanya mazoezi sana.
Mtafiti mkuu Dokta Leah Cahill aliambia BBC: "ujumbe muhimu kwa wote ni kuwa kula kitu asubuhi unapoamka au katika kipindi cha saa moja baada ya kuamka. ''
"matokeo yanaonyesha kitu kodogo ni bora kuliko kutokakula kitu chochote, lakini ni bora kupata lishe bora.''
Alisema kuwa muda ambao mtu anakula ni muhimu na kusubiri hadi nyakati za mchana kabla ya kula chochote ni vibaya kwa mwili wa binadamu.
Aliongeza kuwa hali hii inaweza kusababisha shinikizo la damu mwilini , unene kupindukia na ugonjwa wa kisukari, maradhi yanayoweza kuathiri moyo.
"usikose kiamsha kinywa,'' alisisitiza Dokta Cahill.
Hata hivyo wakosoaji wa utafiti wanasema kuwa , waliwachunguza wanaume pekee na tena wale walio na umri wa miaka 45 na zaidi kwa hivyo itakuwa muhimu kuthibitisha kuwa kukosa kiamsha kinywa kunaweza kuathiri watu wengine walio na umri wa chini ya miaka 45

MTAMBUE MSANII ALIYETANGAZA KUMPORA MUME WA AUNT EZEKIEL... PICHA NA HABARI HIZI HAPA

KATIKA hali isiyo ya kawaida msanii anayechipukia katika filamu za Kibongo, Isabella Fransis ‘Vai wa Ukweli’ anamtafuta ubaya gwiji katika tasnia hiyo, Aunt Ezekiel kwa kusema anamtamani mumewe.


Vai wa Ukweli bila ya kupindisha maneno amedai kuwa hapati usingizi kutokana na kumzimia Sunday Demonte ambaye ni mume wa Aunt.

Akizungumza na mwandishi wetu, Vai alisema ili kuonesha kuwa anachokisema kinatoka moyoni mwake, amekata vipande vya picha za Dimonte na kuvibandika chumbani kwake.

 “Kusema ukweli nampenda sana Sunday na sijaanza kumpenda leo wala jana kwani namfahamu tangu zamani alipokuwa Kariakoo,” alisema Vai.


Msanii huyo chipukizi alisema anamuonea wivu Aunt kwa kuamini kuwa anafaidi sana kwa kuwa na mwanaume huyo.
 
Kwa upande wake Aunt alishangazwa na taarifa hizo na akaomba atafutwe baada ya kumalizika kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili ajue cha kufanya.

Janet Jackson ajiunga na klabu ya mabilionea

Janet-Jackson-is-Married
Mkongwe wa muziki, Janet Jackson, ajipatia nafasi kwenye klabu ya mabilionea kupitia mauzo na shoo za albamu zake kali na kushiriki katika filamu mbalimbali.
Kutoka katika chati za muziki mpaka kwenye fashion, hajawahi kushindwa kuonekana kwa njia moja au nyingine.
Sasa, Janet Jackson ameongezwa kwenye orodha nyingine: mabilionea.
Kwa mujibu wa Variety Magazine, Jackson amejipatia dola milioni 458 kutoka kwenye ziara za muziki na dola milioni 260 kutokana na mauzo ya albamu zake.Vilevile alipokea dola milioni 81 kutoka kwa wadhamini na dola milioni 304 kutoka kwenye uigizaji filamu mbalimbali.
Mwaka jana (2012), alifunga ndoa na bilionea Wissam Al Man kwa siri.
Jackson anaungana na mastaa wengine maarufu na mabilionea wa Hollywood kama vile Oprah Winfrey, steven Spielberg, J.K. Rowling and Sara Blakely.

Photos: Prince William & Kate Middleton’s Royal Baby Boy(Britain’s Little Prince)

royal+baby+boy+photos royal+baby+boy+pic royal+baby+boy+pics royal+baby+boy+pictures royal+baby+photo royal+baby+pictures

Chris Brown ambwaga Karrueche Tran, girlfriend wake mpya.

 Chris Brown and His Girlfriend
Miezi kadhaa baada ya kumbwaga Rihanna, mwimbaji Chris Brown aamua kumbwaga girlfriend wake mpya, Karrueche Tran.
Mwimbaji huyo amedai sababu ya kuachana na girlfriend wake huyo mpya ni kwamba kwa sasa anahitaji kuwa single ili kuweka mawazo yake yote kwenye kazi yake ya muziki.
Alipohojiwa na Hollywood Life, Chris Brown alisema;
“Mashabiki zangu wamekuwa wakiniona kwenye mahusiano ya kimapenzi na wasichana tofauti tofauti, mnawajua ni akina nani, lakini kwa sasa mimi kama mwanaume mwenye miaka 24, nimeamua kuwa single.”
“Bado nina urafiki nao mzuri. Kwa sasa nimeamua kuweka umakini wote kwenye muziki wangu kwani niko kwenye kiwango changu cha juu kwa sasa.”

Japan wagundua tiba ya uso kwa kutumia konokono.

snail facial eewww
Saluni ya urembo huko Tokyo inatoa huduma ya kutibu ngozi ya uso kwa kutumia konokono.
Mtaalamu anayetoa huduma hiyo anadai kuwa ute wa konokono hao huondoa ukavu wa ngozi, kuondoa ngozi iliyokufa na kufanya uso uwe mng’aavu na laini kupindukia.Ute wa konokono hao una mchanganyiko wa proteins, antioxidants and hyaluronic acid ambazo huzuia uso kuzeeka.
Tiba hii hudumu kwa muda wa saa 1 ambapo mteja husafishwa uso na kukandwa kabla ya kuwekewa usoni konokono 5 wa salon hiyo.Huduma hii hutolewa kwa takribani dola 245, huwa inajumuishwa na masks na

Mtu mzima Dj Khaled ameshindwa kukaa na la moyoni kwa muda mrefu sasa ameamua aweke wazi kuwa anataka kumchukua jumla jumla (kumuoa) Nicki Minaj na yupo tayari kwani anujua yeye ndiye mwanaume anaefaa kuwa na Nicki, Katika maneno yake Dj Khaled alisema alitamani kumwambia ukweli Nicki Minaja tangu mwaka jana ila alishindwa lakini leo ndo kaamua kusema ukweli..

Mtu mzima Dj Khaled ameshindwa kukaa na la moyoni kwa muda mrefu sasa ameamua aweke wazi kuwa anataka kumchukua jumla jumla (kumuoa) Nicki Minaj na yupo tayari kwani anujua yeye ndiye mwanaume anaefaa kuwa na Nicki, Katika maneno yake Dj Khaled alisema alitamani kumwambia ukweli Nicki Minaja tangu mwaka jana ila alishindwa lakini leo ndo kaamua kusema ukweli..

ANGALIA PICHA ALIYOTUPIA MTOTO WA OBAMA ,SASHA OBAMA KWENYE MTANDAO WA FACEBOOK

Michelle Obama and Nelson Mandela.